loyal-worshippers-at-night-in-masjid-al-haram-makkah-hd-hs4ww1x76q1b4wce

TWENDE HIJJA NA UMRA PAMOJA

Ukiwa MAKKA, utaweza kufanya ibada ya Umra za Sunna kwa wingi

Ukiwa MADINA, utaweza kufanya ibada ya Sunna ya kusali sala 40 za jamaa. Pia, utaweza kufanya ziara kwenye maeneo mengi ya kihistoria na yenye athari kidini ndani na nje ya Madina

Bofya kujua zaidi
ahlusnna

KUHUSU SISI

Ahlu Sunna Wal Jamaa Hajj and Umra Trust ni taasisi ya kidini inayopatikana Zanzibar, Pemba na Dar es Salaam. Taasisi hii inawawezesha na kuwarahisishia mahujaji  kwenda Saudia Arabia (Makka na Madina) kwa ajili ya Hijja na Umra kila mwaka. Tunajivunia uzoefu wa zaidi ya miaka 13 sasa, ubora na uhakika wa huduma zetu.

Bofya kujua zaidi

DHAMIRA YETU

Sisi, taasisi ya Ahlu Sunna Wal Jamaa Hajj and Umra Trust tunakuhakikishia unafanya ibada za Hijja na Umra kila mwaka bila changamoto zozote kama vile malazi, ibada na afya, huku ukifurahia ziara kwenye maeneo matakatifu na ya kihistoria. 

Bofya kujuza zaidi
pexels-mloky96-36704

KINACHOTUFANYA KUWA BORA

TUNAJALI IBADA YAKO

Ukiwa Madina na Makka, utaishi kwenye nyumba karibu na misikiti mitakatifu. Utachinjiwa mnyama wa udhihia kisheria. Uongozi madhubuti katika kutekeleza ibada za HIjja na Umra. Tunatoa Ihram kwa wanaume na wanawake, pamoja na Khanga.

TUNAJALI AFYA YAKO

Tunatoa matibabu bora wakati wote ukiwa safarini na Saudia Arabia. Upatikanaji rahisi wa "Wheel Chaiir" kwa maombi. Upatikanaji wa chakula bora (milo mitatu kwa siku) kwa utaratibu wa "Buffet" na vyakula maalum kwa wagonjwa (Special Diet).

TUNAJALI FURAHA YAKO

Tunahakikisha kuwa safari yako kuwa yenye furaha kila wakati. Tunakupatia begi moja la kusafiria, zawadi ya maji ya Zamzam, tunakupatia mahema (tents) yenye ubora unapokuwa Mina na Arafa. Utafanya ziara sehemu takatifu na za kihistoria (Madina, Makka na Badri).

KWA NINI UTUCHAGUE SISI

Taasisi yetu imekuwa na huduma bora inayoendelea kukua kila mwaka, ubora wa uendeshaji huduma, timu ya wataalam, upatikanaji wa msaada wakati wote, matokeo bora ya kuridhishwa kwa huduma kutoka kwa wateja wetu na utayari wa kukusikiliza na kukushauri inapohitajika.


UBORA WA UENDESHAJI HUDUMA

Kwa zaidi ya miaka 13 tumekuwa tukihakikisha ubora wa huduma ndiyo kipaumbele chetu. Baadhi ya uboreshaji umehusisha uandaaji wa semina kabla ya kwenda hijja, ugawaji wa vitabu na vipeperushi kuhusu hijja na megine zaidi.

Bofya kujua zaidi
TAASISI INAYOENDELEA KUKUA KILA MWAKA

Taasisi yetu imeendelea kukua na kuwafikia wateja wetu kwa ukaribu zaidi. Kupitia ofisi zetu zilizopo Zanzibar, Pemba na Dar es Salaam, tumeendele kuhakikisha tunakufikia kwa ukaribu na kukudumia kwa urahisi zaidi. Hii ni pamoja na kukuwezesha kuanza safari za ndege kutokea Zanzibar, Pemba au Dar es Salaam. Kupata usafiri wa uhakika ndani ya Saudia Arabia. Pia, mawakala wetu waliopo mikoani wamekuwa msaada katika kufanikisha huduma zetu kuendela kukua na kukusogelea karibu zaidi.

Bofya kujua zaidi
TIMU YA WATAALAM KWENYE HUDUMA

Kila wakati tumehakikisha kuwa na wafanyakazi wenye utayari wa kukuhudumia kwa ubora. Wataalam wetu watakuwa nawe bega kwa bega kwenye hatua zote hapa Tanzania na ukiwa Saudia Arabia. Wataalam watakuelekeza yote upaswayo kuyafahamu wakati wote wa kuanzia mwanzo hadi mwisho wa safari yako.

Bofya kujua zaidi
1+
JUMLA YA IDADI YA SAFARI ZA HIJJA NA UMRA HADI SASA
1+
IDADI YA MAHUJAJI TULIOWAHUDUMIA HADI SASA
1+
JUMLA YA IDADI YA WAFANYAKAZI
1+
JUMLA YA MIAKA YA UZOEFU
Scroll to Top